Tuesday, October 25, 2016

TUMEKUWA CHAWA WAO VYA KUTOSHA SASA TUNAKWENDA KUWEKA HADHARANI KILA KITU


STAA wa filamu za kitanzani Jimmy Mafufu ameonyesha  hisia zake  kutokupendezwa na aina ya mfumo wa usambazaji unaotumiwa kwani  umekuwa ukiwagawa pande mbili tofauti
Mafufu amabaye ni Mkurugenzi  mtendaji  wa  J mafufu The Strong Film ameonyesha hisia zake kwa kuandika ujumbe kupitia ukurasa wake wa facebook
kwa mujibu  Mafufu Kupitia ukurasa wake aliandika
" nawaonea huruma sana waigizaji wa mikoani tasnia imejaa ubinafsi mkubwa wasambazaji nao ni tatizo lingine kubwa wameendelea kuwagawa waigizaji ili wawatawale hawataki sura mpya kabisa lakini cha ajabu ninaowaonea huruma nao hawana umoja wanachukiana wao kwa wao hawakubaliani hata chembe kila mmoja anajua kuliko mwingine ni maombi yangu mungu awape macho ya rohoni waigizaji wote wa mikoani ili mkipewa macho hayo muisaidie tasnia hii kukua zaidi msichokijua ni kwamba tasnia inawategemea sana lakini mkiacha upuuzi wa kuchukiana na kutokukubaliana”
kwa msisitizo mafufu aliongeza
"muda umefika wa kila muigizaji tanzania kuliishi jasho lake hatuwezi kunyamaza wala kuendelea kumsujudia mtu anayetugawa ili atutawale yeye anakuwa tajiri kupitia filamu zetu sisi tunazidi kuwa masikini na watumwa wake hapana sasa nimejitolea kumfunga paka kengere inatosha sasa ulivyovuna kwa wizi na dhuruma vitunze maana unakwenda kuicha tasnia hii mikononi mwa wenyewe wito wangu kwa waigizaji wote tanzania mkisikia la mgambo limelia msiulize wapi kila mtu afunge kibwebwe tayari kwa kumkabili adui wa tasnia hii ya filamu ambaye mimi namjua na nitawaonyesha kwa vitendo muda sio mrefu muigizaji hawezi kuwa masikini duniani kote unaweza kuishi kifalme kwa filamu yako moja tu kifo cha kanumba na sajuki kiwe funzo lazima familia zetu zije ziishi vizuri siku tukiondoka duniani sio wahindi ndio wawe matajiri kupitia kazi zetu harafu familia zetu ziwe omba omba no no no sasa nakinukisha na nilishatoa angalizo mapema huwa sitaniii na sijasomea kushindwa mumeiibia sana serikali mumewaibia sana wasanii mumetugawa ili mututawale sasa inatosha nitatoka jasho la chuma ili waigizaji kila mahali tanzania waliishi jasho lao nimechaguliwa na kuaminiwa na waigizaji kuwa makamu mwenyekiti wa chama cha waigizaji tanzania na sasa nataka kuonyesha kwa nini nimekuwa kiongozi kwa vitendo anzeni kufungasha vilivyo vyenu kabla hamjaozea jela"
Mpaka  tunakufikishia habari hii Mafufu ameandika  ujumbe mwingine leo alfajiri akisema
"mapinduzi makubwa katika tasnia ya filamu yanakuja kila mwanafani mahali popote alipo tanzania atanufaika kupitia kipaji chake huyu mnyonyaji muda wake wa kufungasha virago vyake umetarajadi waigizaji anzeni kujiimarisha kisanaa na kuongeza weredi ili kuboresha kazi za sanaa naelewa tumewapoteza waigizaji wengi wazuri na wenye vipaji vya hali ya juu kutokana na ukilitimba wa wasambazaji uchwara tumegawanywa vya kutosha sasa kimenuka na soon la mgambo litapigwa kila muigizaji ajiandae tumechoka kumtumikia kafili.vipaji ni vyetu filamu ni zetu na tanzania ni yetu wametuchezea vya kutosha na tumekuwa chawa wao vya kutosha sasa tunakwenda kuweka hadharani kila kitu"

baadhi ya wadau wa filamu na waigizaji hasa walio chini walionyesha hisia zao kwa kutoa yao ya moyoni
Haidari Saidi Chumambili Mungu akusimamie Mwalimu Wangu maafufu umekuwa so tu mwanaharakati Bali mwenye kupigania mabadiriko ya kweli. Mungu awe nawe
Nai Nicholaus Go ahead na mungu atasimamia hilo...
Lunyiliko Kiyaulilo hatutakuwa nyuma yako kwa mapambano, bali tutakuwa bega kwa bega kiongozi wetu. na mungu atatusimamia maana anaona jitihada zinazofanyika. mungu yuko nasi

www.didasentertainment bado inaendelea na harakati za kumtafuta staa huyo kwa habari zaidi tutakufahamisha endelea kuwa nasi karibu

No comments:

Post a Comment