Sunday, May 1, 2016

MSIBA MWINGINE MKUBWA WAIKUMBA BONGO MOVIES

BONGO MUVI IMEKUFA AU NI MANENO YA MTAANI TU?
Juzi nimeshituka sana baada ya rafiki yangu mmoja kuniambia kuwa kama kuna super star ambaye anauwezo wa ku produce filamu na yupo ana shoot filamu kwa sasa ni mtajie jina kama wapo hawazidi wawili! Nilishituka nikajiuliza kwa nini? Nikapata shida sasa huenda Bongo muvi imekufa! Nikaanza kufanya uchunguzi nikakuta kila producer ana shoot tamthilia. Haa nilishangaa mastar waliotoka kwenye tamthilia wakiita ni maigizo wakaenda kushoot filamu ambazo pia hazikuwa na tofauti na maigizo wakirudi kufanya maigizo. Duuuh! Nikaanza kujiuliza maswali bila majibu.
Hivi wadau ni wapi tumekosea? Ni msanii, mzalishaji, msambazaji au mnunuzi wa mwisho kachoka? Taratibu kumbukumbu zangu zikanirudisha miaka minne iliyopita kabla Steven Kanumba hajafa ambapo struggle za wasambazaji kumiliki wasanii ma star zilivyo pamba moto na mastar kutoa vikwazo kwa waandaaji wadogo. Maana ulikuwa ukienda kutaka kufanya kazi utajibiwa na mkataba steps mwingine na mkataba pilipili basi tu ilikuwa vituko na wasio na mikataba pia walisema na wao wanamikataba mhuuu!
Nikakumbuka kipindi kizuri cha ushindani. Kipindia ambapo tulikuwa na wasambazaji wa kutosha. Tulikuwa na Steps na Kapico pia kulikuwa na Pili pili, Vishal na Famous Video, Ajay, Bajomba, Game 1st Quality, Churu Peace, Mwananchi, Al- Liyamy, SAS"O" Splash, Gibs Video, Tolly wood, Papazi, Proin, Whatever, GMC Wasanii,Beck Net, Criss Creation n.k hizi zote zilikuwa na ushindani na kila kampuni ilitoa muvi moja kwa wiki. Kampuni hizi zilikuwa ni kubwa na zilileta changamoto na kulifanya game liwe hot. Na kama inavyojulikana kwenye ushindani yule mwenye mtaji mkubwa aliwashinda wenzake. Akatumia mbinu zake kuteketeza wenzake leo hii ule ushindani haupo si hakuna wengine, utashindana na nani bidhaa inatoka sehemu moja. Mtu anataka awe peke yake! Radha ikapungua kwa watazamaji watu wakawa wanafanya kazi kuwahi foleni si hakuna kwingine pa kuuza.
Sasa mawazo yangu yakanirudisha ni nani kaua soko? Unapeleka muvi leo inatoka baada ya miaka miwili! Kumbe ungepeleka kwenye kampuni nyingine na ungeuza mapema! Duuh zile siku za ushindani zilikuwa nzuri ndio maana maneno midomoni yakawa mengi watu wakiisifia na kila mtu akahamasika kuwa msanii kwa nafasi yake.
Ukitazama kabla ya Kifo cha Steven Kanumba kulikuwa na kampuni nyingi sana za usambazaji tena zenye uwezo mkubwa ila baada ya kifo chake kampuni moja moja ikaanza kupoteza uwezo wa kusambaza na kuishia kufunga kampuni. Wakabaki wasambazaji wachache ambao walijikongoja na mpaka sasa msambazaji akitoa muvi tatu unatakiwa kumheshimu wengi huishia mbili tu chali. Mungu atunusuru! Swali ukitengeneza muvi unauza wapi? Mbona wasanii mastar wanakimbia kufanya muvi? Kuna tatizo gani? Au ndio upepo wa kukurupuka umeenda kwenye tamthilia? Au ni kwa sababu TV stations zimeongezeka? Midomoni mwa maproducer wengi ni ku produce tamthilia kitu ambacho kinahitaji bajeti kubwa kuliko muvi!
MUNGU BARIKI TASNIA YETU.

No comments:

Post a Comment