Tuesday, May 3, 2016

Vilio vilitawala jana wakati zaidi ya nyumba 400 za wakazi wa Mtaa wa Mloganzila,Kibamba katika Manispaa ya Kinondoni, Dar es Salaam, zilipokuwa zikibomolewa.Ubomoaji huo ulianza saa 4:00 asubuhi baada ya mmiliki wa eneo hilo la ekari 33, Henry Kashangaki kushinda kesi dhidi ya watu 11 wanaodaiwa kuvamia eneo hilo na kuwauzia wananchi wengine ambao walijenga nyumba bila kufahamu undani wa eneo hilo.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti baadhi ya waaathirika wa ubomoaji huo, walisema taarifa za kutakiwa kuondoka katika eneo hilo kabla ya kuvunjiwa nyumba zao, walizipata Aprili 30 mwaka huu na hawakupewa muda wa kutosha kuondoa mali zao.
Mkazi mmoja ambaye hakutaka jina lake lijulikane, alilalamikia kuwa hawakutendewa haki kwa vile haikuwa rahisi kwa muda huo mfupi wa siku moja kuweza kuokoa mali zao.

No comments:

Post a Comment